. BIMA YA NYUMBA au MALI; MASWALI 5 KABLA YA KUKATIA ~ Covenant Company (T) Limited

Ads

9.7.21

. BIMA YA NYUMBA au MALI; MASWALI 5 KABLA YA KUKATIA

Posted By: Covenant Company (T) Limited - 18:52


Bima ya Nyumba

BIMA YA NYUMBA / MALI: MASWALI 5 KABLA YA KUKATA

Nani anaweza kukatia Nyumba au Mali zake Bima?

Ni mtu ambaye ni mmiliki kisheria wa Nyumba hiyo au Mali hizo na ambaye kama majanga yakitokea yeye ndio atakayepata hasara za kifedha. Mali zinaweza kuwa vitu binafsi au mali za mfanyabiashara mfano wafanyabiashara (maduka yao), n,k.

Je nitanufaikaje?

Bima itakupatia fidia dhidi ya hasara au uharibifu utokanao na:

  • Majanga ya Moto, mfano kama masoko yaliyowahi kuungua Dar es Salaam, Mwanza, Morogoro, n.k.
  • Majanga ya Mafuriko
  • Majanga ya Tetemeko la Ardhi, mfano yaliyowahi kutokea Kanda ya Ziwa, n.k.
  • Majanga ya Upepo Mkali na Kimbunga.
  • Majanga ya kudondokewa na vitu mbalimbali.
  • Majanga mengine ya Asili.

Bima ya Nyumba inajumuisha Vitu gani?

Bima ya Nyumba itakulinda katika sehemu kuu zifuatazo utakazokatia;
Nyumba yenyewe na ukuta wake ikiwa wewe ni mmiliki wa nyumba.

Bima ya Mali itajumuisha;

  • Vitu vyote vya thamani vilivyomo ndani ya nyumba au jengo la Biashara.
  • Mali zinginezo kama simu, kamera, saa, cheni, mabegi, vinakilishi, Kompyuta, n.k.
Bima ya Mali, inaweza kukatiwa na wafanyabiashara wenye maduka makubwa, saizi yakati au madogo. Muhimu ni kufanya tathimini na kujua mali zako zinathamani ya kiasi gani.

USINGOJEE MAJANGA YATOKEE NDIO UKATIE BIMA MALI ZAKO EWE MFANYABIASHARA.

Gharama ya Bima ya Nyumba ni kiasi gani?

Bima ya nyumba ni gharama nafuu sana na inalipwa mara moja kwa mwaka kuzingatia vitu mbalimbali vitakavyobainishwa muda wa kukatia.

Ada ndogo (Premium) kabisa kwa mwaka ni Tshs 59,000 kwa nyumba yenye thamani ya Tshs 35,000,000# na itakuwa ikiongezeka kadri thamani ya nyumba inavyoongezeka, kwa mfano;

Ada ya Bima ni 0.15% ya thamani ya nyumba yako, Bima zote za mali huchajiwa kodi hivyo utalipia kodi (VAT) ya 18%.

Thamani ya Nyuma (Tshs)

Ada kwa Mwaka (Tshs)

35,000,000

61,950

50,000,000

88,500

75,000,000

132,750

100,000,000

177,000

150,000,000

265,500

200,000,000

354,000

Nahitaji vitu gani vya muhimu ili nikatie Nyumba au Mali Bima?

Hakikisha una kielelezo chochote kile kinachoonesha kuwa wewe ndio mmiliki halal wa nyumba, mfano; Hati ya Nyumba, Bili ya Maji au Malipo ya Luku, Mauziano ya Kijiji, Stakabadhi ya Malipo ya Ardhi, n.k.

Ili kukatia Malizako tutahitaji yafuatayo:
-Kitambulisho chako.
-Mkataba wa Kupanga eneo la biashara / nyumba
-Tutakutembelea na Kupiga Picha ofisi kwa wafanyabiashara.

EWE MFANYABIASHARA TUNAKUSHAURI UKATIE BIMA MALI ZAKO.

Wasiliana na sisi sasa hivi:
Namba za simu: +255 754 233 717
Email: tzcovenant@gmail.com / elinsuranceltd@gmail.com

Covenant Company (T) Limited

Habari, Ni furaha kwetu kukuhudumia Popote ulipo. Tupigie / Call/WhatsApp Us +255754233717 kwa uhitaji wa huduma zetu. Karibu

0 comments:

Post a Comment

© 2016 - 2021 | Covenant Company (T) Limited. All Rights Reserved | Privacy . Terms |

Designed By Kanuti|+255754233717